STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 30, 2014

Chelsea wapata afueni, Terry, Cech warejea dimbani

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Petr+Cech+John+Terry+Blackburn+Rovers+v+Chelsea+jBW-c2W_Ow3l.jpg
Terry na Cech wakipongezana katika moja ya michezo yao
KIPA tegemeo wa Chelsea Petr Cech na nahodha John Terry wanatarajiwa kucheza mechi ya leo na nusu fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya kati yao na Atletico Madrid baada ya wachezaji hao kufanya mazoezi ya timu hiyo tangu juzi.
Ilisemekana Cech asingeweza kucheza tena msimu huu baada ya kuteua bega lake katika mchezo wa kwanza wakati Terry alitolewa nje kutokana na kuumia kifundo cha mguu katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya 0-0. 
Eden Hazard na Samuel Eto’o ambao walikuwa majeruhi wao pia walionekana kuwa fiti kwa kufanya mazoezi  jana, huku viungo John Mikel Obi na Frank Lampard wote hawatakuwepo katika mchezo huo wa marudiano utakaofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge kutokana na kutumikia adhabu ya mechi moja.
Kwa sasa imebaki maamuzi ya kocha Jose Mourinho kuona kama anaweza kuwatumia wachezaji waliorejea toka kwenye majareha kwa ajili ya mechi hiyo kuwania nafasi ya kutinga fainali kuifuata Real Madrid iliyotangulia usiku wa jana kwa kuizabua waliokuwa watetezi, Bayern Munich kwa kwa mabao 4-0.

No comments:

Post a Comment