STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 30, 2014

Bayern chali yapigwa 4-0 kwao na kuvuliwa taji

* Leo zamu ya Chelsea na Atletico Madrid

UNAWEZA usiamini ila ndivyo ilivyo, mabingwa watetezi wa Ligi ya Ulaya Bayern Munich wamevuliwa taji hilo baada ya kukandikwa mabao 4-0 na Real Madrid na kuwafanya wababe hao wa Hispania kutinga fainali.
Mpango wa kocha Carlo Ancelotti wa kuwapanga washambuliaji wake watatu Karim Benzema, Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ulizaa mpango baada ya Real kuisambaratisha Bavarians nyumbani kwao bila kutarajiwa na kuzima ndoto za Pep Guardiola kubadilisha matokeo ya kipigo cha bao 1-0 ilichopewa timu yake katika  mechi ya kwanza.
Mabao mawili ya Sergio Ramos na mengine ya Cristiano Ronaldo yalitosha kukwamisha safari ya wababe hao wa Ujerumani kwenye uwanja wao wa Allianz Arena na kukubali kulitema taji hilo.
Ramos alianza kufunga bao la kwanza dakika ya 16 kwa pasi ya Luka Modric kabla ya kuongeza jingine dakika nne baadaye akimalizia pasi ya Pepe na Ronaldo alikuja kupigilia msumari katika dakika ya 34 kwa pasi ya Bale na kumalizia udhia dakika ya 90 kufunga bao la nne.
Real Madrid sasa inasubiri mshindi kati ya Chelsea ya England na Atletico Madrid wanaoumana leo katika mechi ya marudiano nyingine ya nusu fainali, mechi itakayochezwa mjini London.
Katika mechi ya kwanza timu hizo ziliotoka suluhu ya kutofungana na yeyeote eatakayetumia vyema karata yake ataifuata Real kwenye fainali ya Mei 24 mjini Lisbon Ureno.

No comments:

Post a Comment