STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, April 30, 2014

Malawi yatua kuifuata Stars Mbeya

http://www.malawidemocrat.com/wp-content/uploads/2012/06/Flames-e1339493490888.jpg
Malawi the Flames wanaotua leo kuivaa Taifa Stars
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXy4DjvygUby0tzSChTVErun58_E3LDqa5xJ_i2zWfMLszWFaSyC9gFEfrYDK13Z3ay7OtaoFftdVKgyeW0ng6kOwB9SLKwda42hmSDnjKljVaRMR3dk2Wg9ugd3lFENkSbBF8-a-GegEK/s1600/FKB_1718.JPG
Taifa Stars itakayoikaribisha Malawi ikiwa na kocha mpya Mart Nooij
TIMU ya soka ya taifa ya Malawi (Flames) inatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili hii kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya.
Boniface Wambura, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), alisema jijini Dar es Salaam  kuwa Flames yenye msafara wa watu 31 utakaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Soka cha Malawi (FAM) itaingia Mbeya kwa usafiri wa barabara. Wachezaji katika msafara huo watakuwa 20.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya tangu juzi kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano ya kuwania kufuzu fainali zijazo za Afrika (AFCON) dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.
Mwishoni mwa wiki Taifa Stars iliyofinyangwa na TFF, ilitia doa sherehe za miaka 50 ya uwapo wa Tanzania baada ya kuchapwa  magoli 3-0 dhidi ya timu ya taifa ya Burundi (Intamba Murugamba) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment