STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 27, 2014

Manchester City yatakata England

Pole position: Manchester City moved back into the driving seat in the title race with victory at Crystal Palace
Samir Nasir akishangilia bao la Dzeko aliyembeba
Yaya Toure gives Manchester City a 2-0 lead against Crystal Palace at Selhurst Park
Yaya Toure akifunga bao la pili la Man City
MBIO za ubingwa wa Ligi Kuu ya England zimezidi kuwa ngumu kutabirika baada ya usiku huu Manchester City kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Crystal Palace na kuijongelea Chelsea iliyoisimamisha Liverpool ikiwa nyumbani jioni ya leo.
Bao la mapema la dakika ya nne lililofungwa na Edin Dzeko na lingine kupitia wa Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure dakika mbili kabla ya mapumziko ziliwafanya vijana wa Manuel Pellegrini kufikisha pointi 77, moja nyuma ya Chelsea yenye 78 na mbili pungufu na zile za Liverpool yenye pointi 80.
Manchester hata hivyo imecheza mechi pungufu zaidi ya wapinzani wao waliosaliwa na mechi mbili kila moja, huku wenyewe wakiwa na mechi tatu kabla ya kumalizia msimu wa ligi hiyo.
Kwa kipigo hicho cha nyumbani Crystal Palace imeendelea kusalia kwenye nafasi ya 11 ikiwa na pointi 43 kutokana na mechi 36.
Kipute cha ligi kitaendelea tena kesho kwa pambano moja tu litakalowakutanisha Arsenal watakaokuwa nyumani kuwakaribisha Newcastle United, wakiwa katika mbio za kujihakikisha nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani wakichuana na Everton ambayo jana ilifungwa na Southampton ikiwa kwao.

No comments:

Post a Comment