STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 27, 2014

PSG yabaki kidogo kutetea taji la Ligi Ufaransa

http://images.football365.com/13/09/800x600/PSG-v-Toulouse-Edinson-Cavani-celeb_3011490.jpg
Cavani aliyeitanguliza PSG kwenye taji la Ligue 1 nchini Ufaransa
KLABU ya PSG ya Ufaransa inaelekea kunyakua ubingwa wa ligi ya nchi hiyo kwa mara ya pili wakati huu ikiwa uwanjani ikiongoza bao 1-0 ugenini dhidi ya Sochaux.
Mechi ikiwa inaelekea mapumziko, PSG imebakiza hatua chache kabla ya kunyanyua juu ubingwa wa nchini baada ya Edinson Cavani kutupia bao dakika ya 25.
Kabla ya mechi hiyo PSG ipo kileleni ikiwa na pointi 82, ikiwaacha wapinzani wao wa karibu Monaco ambayo jana ilipata ushindi wakiwa na pointi 75 na kusaliwa na mechi tatu ambazo kama itashinda itakusanya jumla ya pointi 84 tu ambazo kama PSG itashinda leo itakuwa imezivuka na hakuna wa kuweza kuzifikia pointi zake 85.
MICHARAZO itawaletea taarifa zaidi kujua kama matajiri hao wa Paris wameweka kibindoni taji hilo wakiwa bado na mechi tatu mkononi.

No comments:

Post a Comment