STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, April 27, 2014

Sunderland 'yaua' England yatoka mkiani

Sunderland striker Connor Wickham (left) watches as his header puts his side in front against Cardiff
Sunderland ilipokuwa ikijitetea EPL muda mfupi uliopita
VIBONDE wa Ligi Kuu ya England, Sunderland ikiwa uwanja wao wa nyumbani wa Stadium of Light imefanya mauaji ya kutisha baada ya kuigagadua Cardiff City kwa mabao 4-0. huku wageni hao walicheza pungufu kwa nusu nzima ya mchezo huo kwa kuonyeshwa kadi nyekundu..
Sunderland iliyokuwa mkiani ilichupa hadi nafasi ya 17 kwa kufikisha pointi 32 ilipata ushindi huo wa pili mfululizzo baada ya wiki iliyopita kuinyuka Chelsea na kuiacha Cardiff wakiwapokea kwenye nafasi hiyo katika hatari ya kushuka daraja.
Ushindi huo wa Sunderland uliopatikana muda mfupi uliopita kupitia mabao ya Conor Wickham aliyefunga mabao mawili katika dakika ya 26 na 86, huku jingine lililokuwa la pili likifungwa na Fabio Borini kwa mkwaju wa penati dakika za nyongeza kabla ya timu kwenda mapumziko.
Bao jingine lililoisaidia timu hiyo kufikisha jumla ya pointi 32 wakati mechi ligi ikielekea ukingoniu lilifungwa na Muitaliano Emanuele Giaccherini dakika ya 76.

No comments:

Post a Comment