STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, January 11, 2014

Simba yavunja mwiko, Kiemba we acha tu

 
AMRI Kiemba amezidi kudhihirisha kuwa yupo kikazi zaidi kama alivyopwahi kunukuliwa na Blogu hii baada ya usiku wa jana kuhusika na mabao mawili yaliyotosha kuvunja mwiko wa URA wa kutofungwa na Simba kwenye mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi.
Kiemba, alitengeneza bao la kwanza lililofungwa na beki Joseph Owino kabla ya kuongeza jingine na kuipa Simba ushindi wa mabao 2-0 na kuivusha hadi Fainali ya michuano hiyo.
Mabao yote mawili yalifungwa kwenye kipi8ndi cha pili baada ya kipindi cha kwanza kuisha timu zikiwa hazijafungana na URA wakicheza punguyfu baada ya nyota wao Oweni Kasule kutolewa kwa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Ramadhani Singano 'Messi'.
Kwa ushindi huo asmbao umeifanya Simba kuweka rekodi kwa kuondoa uteja kwa URAnma kutinga Fainali bila kupoteza mchezo zozote wala kufungwa bao lolote katika lango lao, limeifanya Simba sasa kukutana na KCC ya Uganda iliwatemesha taji waliokuwa watetezi, Azam.
Azam walikumbana na lkipindi cha mabao 3-2 katika mechi ya kwanza iliyochezwa jioni kwenye dimba la Amaan licha ya kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-1, mabaoi yake yakiwekwa kimiani na kinda, Joseph Kimwaga.
Fainali ya michuano hiyo itachezwa Jumatatu kwenye uwanja huo wa Amaan.

No comments:

Post a Comment