STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 10, 2014

Hapatoshi Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi leo

Kikisi cha Simba kitakachovaana na URA

Watetezi Azam watakaovaana na KCC

LEO ni kimbembe katika Nusu Fainali ya Kombe la Mapinduzi wakati Azam itavaana na KCC ya Ungada wakati Simba ikishuka dimbani usiku kuivaa URA.
URA imekuwa ikiionea Simba kila wanapokutana nao kwa muda mrefu sasa iwe kwenye mashindano au mechi za kirafiki na kufanya mechi hiyo kuwa yenye mvuto zaidi kuliko ya KCC na watetezi Azam.
Hata hivyo mechi zote zinaonekana kusisimua kutokana na ukweli inazikutanisha timu za Tanzania na Uganda ambazo timu zao za taifa zimekuwa zina upinzani katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Simba ilitinga nusu fainali baada ya kuibamiza mabao 2-0 timu ngumu ya Chuoni FC ya Unguja katika mchezo wa robo fainali uliopigwa kwenye Uwanja wa Amaan usiku wa kuamkia jana na URA URA ikifuzu baada ya kuifunga KMKM bao 1-0 kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba juzi.
Azam ambayo haijapoteza mchezo wowote katika michuano hiyo mpaka sasa itataka kuitoa nishai KCC ili kuweza kutinga fainali na kusubiri kuona itaumana na nani Jumapili kutetea taji lake.
Simba wenyewe itawavaa URA ikimtegemea nyota wake Ramadhani Singano 'Messi' na wakati wengine walioipaisha timu hiyo kwenye michuano hiyo.
Messi alifunga mabao mawili katika mechi ya robo fainali na kuibuka mchezaji bora wa michuano hiyo, japo Mrundi Amissi Tambwe ameling'ang'ania moja ya mabao hayo akidai alifunga yeye.
Makocha wa timu zote nne zilizotinga nusu fainali wamenukuliwa visiwani humo wakitamba kuwa wapo tayari kwa vita ili kuona vikosi vyao vikitinga fainali na hatimaye kunyakua taji hilo.
Tangu michuano hiyo ilipoanzishwa, hakuna klabu kutoka nje ya Tanzania imefanikiwa kutwaa taji hilo na hivyo Simba na Azam kuwa na mtihani wa kuhakikisha zinakutana tena zenyewe kwa zenyewe kulinda rekodi.

No comments:

Post a Comment