STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 10, 2014

Yaya Toure atwaa tena tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika


KIUNGO nyota wa klabu ya Manchester City na timu ya taifa ya Ivory Coast, Yaya Toure ametawazwa kwa mwaka wa tatu mfululizo kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika.
Yaya aliwashinda Mnigeria John Obi Mikel aliyeshika nafasi ya pili na Didier Drogba.
Toure, aliyeshinda tuzo hiyo mwaka 2011 na 2012, alipata kura 373 dhidi ya 265 na 236 za Mikel na Drogba waliomfuatia.
Sherehe za utoaji tuzo hiyo na nyingine zilihudhuriwa na Maofisa mbalimbali wakiwemo Rais wa CAF, Issa Hayatou, Gavana wa Lagos, Babatunde Fashola Raji Fashola, Waziri wa Vijana na Michezo Nigeria, Alhaji Bolaji Abdullah, Wajumbe wa Kamati Kuu ya CAF na wengineo.
Kwa tuzo ya mchezaji bora anayecheza Afrika, ilienda kwa kiungo wa Misri, Mohamed Aboutrika aliwashinda  Ahmed Fathy  wa Misiri na Sunday Mba wa Nigeria.
Hiyo ilikuwa mara ya nne, Aboutrika, aliyetangaza   kustaafu soka hivi karibuni kushinda tuzo hiyo akifanya hivyo mwaka 2006, 2008 na 2012.

TUZO ZA CAF ZILIZOTOLEWA JANA:

Mchezaji Bora wa mwaka; Yaya Toure, Ivory Coast na Manchester City
Mchezaji bora wa mwaka anayecheza Afrika; Mohamed Aboutrika, Misri na Al-Ahly
Mwanasoka anayechipukia; Kelechi Iheanacho (Nigeria)
Timu bora ya mwaka; Nigeria
Timu bora ya vijana ya mwaka; Nigeria U-17 klabu bora ya mwaka; Al-Ahly (Misri)
Kocha bora wa mwaka; Stephen Keshi (Nigeria)
Refa bora wa mwaka; Haimoudi Djamel (Algeria)
Tuzo ya mchezo wa kiungwana; Mashabiki wa Nigeria
Magwiji wa CAF; Bruno Metsu, Mehdi Faria
Tuzo ya Platinum; Goodluck Jonathan (Rais wa Nigeria)
11 bora wa kuunda kombaini ya Afrika;
Kipa: Vincent Enyeama (Nigeria)
Mabeki: Ahmed Fathy (Misri), Mehdi Benatia (Morocco), Kevin Constant (Guinea)
Viungo: Jonathan Pitroipa (Burkina Faso), John Obi Mikel (Nigeria), Yaya Toure (Ivory Coast), Mohamed Aboutreika (Misri)
Washambuliaji: Emmanuel Emenike (Nigeria), Asamoah Gyan (Ghana) na Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon).

Mara baada ya kupokea tuzo yake Yaya amewashuku kaka zake,Obi Mikel na Drogba.

No comments:

Post a Comment