STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 9, 2014

Kiemba yupo kikazi zaidi Msimbazi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiEps_zFlpFfrIRTHTU257hsjXqtA3uCzF1EGsUAwBerMzrMu3p71BRHrvT_PAW8jmgbx_rRosYweFvnR2QgN-fg9FuvtsrJH864KdBbmabBo26I2G3mMzDW-LOY6-JuP35XAxWAxMRf5Q/s640/AMRIKIEMBASIMBA.jpg
Amri Kiemba kishangilia moja ya mabao yake
 KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Amri Kiemba, amesema kwa sasa hana muda wa kupiga blabla kwenye vyombo vya habari na badala yake anaelekeza ngumu na kuwaonyesha mashabiki wa kandanda kipi anachokifanya uwanjani.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu toka Zanzibar, Kiemba alisema anaamini wote ambao walikuwa na maoni tofauti dhidi yake watakuwa wamepata salama kutokana na kile anachokifanya.
Kiemba alisema kutokana na hilo kwa sasa ameamua kufunga mdomo wake kuzungumza lolote badala yake kufanya kazi kwa manufaa ya klabu yake.
"Dah kwa sasa nimeamua kukaa kimya ili nifanye kazi, naamini hivi ndivyo inavyotakiwa ili kuwafanya watu wapime kazi yangu uwanjani na siyo kwenye vyombo vya habari," alisema Kiemba.
Mchezaji huyo ambaye magoli yake mawili aliyoyafunga kwenye mechi mbili tofauti yaliisaidia Simba kuvuka hatua ya robo fainali ya mashindano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar.
Kiemba alifunga bao la kwanza wakati Simba ikiilaza AFC Leopards katika mechi ya kwanza ya kundi B kabla ya kuifunga pia KMKM ya Zanzibar.
Nyota huyo wa zamani wa Kagera Sugar, Yanga, Miembeni na Moro United, alikuwa katika hatihati msimu huu kuondoka Simba kabla ya kupewa mkataba wa miaka miwili baada ya kuzima uvumi alikuwa akielekea Yanga.
Klabu hiyo ya Simba jana ilifanikiwa kuinyuka Chuoni katika mechi yao ya Robo Fainali ya Mapinduzi kwa mabao 2-0 na sasa wanakutana na timu inayowasumbua kwa muda mrefu ya URA toka Uganda.
Simba kwa miaka zaidi ya miwili ikikutana na URA imekuwa ikitepeta, japo ukali wa kocha Zdrakov Logarusic na msaidizi wake, Suleiman Matola wanatoa matumaini ya kupata dawa ya kuizima URA kab la ya kujua itavaana na nani kati ya Azam na KCC ya Uganda.

No comments:

Post a Comment