STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 9, 2014

Jennifer Mgendi aachia video mpya iitwayo 'Hongera Yesu'

MUIMBAJI nyota wa muziki wa nyimbo za Injili, Jennifer Mgendi ameibuka na albamu mpya ya video iitwayo 'Hongera Yesu' yenye nyimbo saba.
Akizungumza MICHARAZO, Mgendi alisema kuwa albamu hiyo tayari imeshatua madukani na aliwataka wapenzi wa muziki huo kutonunua CD 'feki' kwani kufanya hivyo kunawavunja moyo wasanii.
Video hiyo mpya mbali na kibao cha 'Hongera Yesu' kilichobeba jina la albamu, pia ina nyimbo kama 'Nikufanyie Nini?', 'Kikulacho', 'Mimi ni Wako', 'Baraka Zangu', 'Fumbua Macho' na 'Msimamo'.
Katika nyimbo za albamu hiyo Mgendi amewashirikisha nyota wengine wa muziki wa Injili kama Bahati Bukuku, Bonny Mwaitege, Christina Matai na Martha Ramadhani.
Mbali na kutoa video, Mgendi pia ametoa albamu ya audio ya vibao hivyo, ambayo nayo tayari iko madukani.
Muimbaji huyo amewahi kutamba na albamu kadhaa zilizomtangaza vyema kwenye ulimwengu wa muziki wa miondoko hiyo ikiwamo ile ya 'Mchimba Mashimo' iliyokuwa na nyimbo kama 'Moyo Tulia', 'Nalia', 'Baba ni Wakuaminiwa', 'Niongoze Safarini' na 'Rudi Nyumbani'.
Aidha, Mgendi alisema kuwa mwaka huu anatarajia pia kuzindua filamu yake mpya ambayo hata hivyo hakupenda kuitaja jina kwa sasa kwavile bado ni mapema.

No comments:

Post a Comment