STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 9, 2014

Tom Olaba akimwagia sifa kikosi cha Ruvu Shooting

http://images.supersport.com/AFC-Tom-Olaba-300.jpg
Tom Olaba

KOCHA Mpya wa klabu ya Ruvu Shooting, Mkenya Tom Olaba amekimwagia sifa kikosi cha timu yake akidai kina wachezaji wenye vipaji na uwezo mkubwa wa soka na kudai wanampa imani ya kufanya nao vema katika Ligi Kuu.
Aidha kocha huyo wa zamani wa Mtibwa Sugar, alisema amebaini udhaifu wa aina tatu katika kikosi hicho na kueleza ameanza kurekebisha ili kuwahi pambano lao la kwanza la duru la pili la Ligi Kuu dhidi ya Prisons.
Akizungumza na MICHARAZO, Olaba aliyetua Ruvu Shooting kuziba nafasi ya kocha Charles Boniface aliyehamia Yanga, alisema kwa siku chache tangu aanze kukinoa kikosi chake amebaini kimejaliwa 'vijana wa kazi'.
Olaba alisema asilimia kubwa ya wachezaji wa timu hiyo wana vipaji na uwezo mkubwa wa soka kitu kinachomtia moyo kwamba watafanya kazi kwa ufanisi na kuipaisha Ruvu kwenye duru la pili la ligi kuu.
"Kwa kweli ndiyo kwanza nina siku kama tata au nne tangu nianze kuinoa timu yangu, nimebaini vipaji na vijana wenye uwezo wa soka kitu kinachonitia moyo na kuamini tutafanya kazi vyema," alisema.
Olaba alisema pamoja na vipaji na uwezo wa kisoka, amebaini mapungufu matatu katika kikosi hicho na tayari ameanza kuyafanyia kazi kuyarekebisha.
"Wachezaji hawana uwezo wa kukaa na mipira, kutoa pasi na kunyang'anya mipira, kitu ambacho nimeanza kufanyia kazi mapema ili hata tukienda Mbeya kuvaana na Prisons tuwe tumekamilika, ila nimevutiwa na aina ya wachezaji walipo Ruvu kwani wanajua soka na wana vipaji," alisema.
Ruvu Shooting iliyomaliza duru la kwanza ikiwa kwenye nafasi ya saba kwa kujikusanyia pointi 17 kutokana na mechi 13, imemnyakua Olaba kwa mkataba wa muda mfupi wa miezi sita kwa ajili ya mechi za duru la pili.

No comments:

Post a Comment