STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 9, 2014

Negredo apiga hat trick, Man City ikiigonga West Ham x6

MSHAMBULIAJI Alvaro Negredo usiku wa jana alifunga mabao matatu (hat trick) wakati Manchester City ikiisambaratisha West Ham United kwa mabao 6-0 katika pambano la Nusu Fainali ya Kombe la Ligi.
Negredo alifunga mabao hayo mawili kipindi cha kwanza katika dakika ya 12, 26 na la tatu kipindi cha pili kwenye dakika ya 49.
City waliokuwa uwanja wao wa nyumbani wa Etihad, walienda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-0 bao la tatu lilifungwa na Yaya Toure dakika ya 40.
Kipindi cha pili mbali na bao la Negredo, Edin Dzeko aliongeza mengine mawili kwenye dakika za 60 na 89 na kuifanya City kunusa fainali za michuano hiyo.
Japo soka linadunda, lakini itakuwa kibarua kigumu kwa West Ham kuilaza City ikiwa nyumbani kwake Upton Park mabao 7-0 katika mechi ya mkondo wa pili wiki mbii zijazo.
Nusu fainali ya kwanza iliyochezwa juzi ilishuhudia Manchester United ikizabuliwa mabao 2-1 ugenini na Sunderland.
 

No comments:

Post a Comment