STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 2, 2014

Yaya Toure 'anusa' tuzo nyingine Afrika


CAPE TOWN, Afrika Kusini
YAYA Toure anatarajiwa kutangazwa kuwa Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Afrika na kuifikia rekodi ya kuibeba tuzo hiyo mara tatu mfululizo baada ya kutajwa katika orodha ya wachezaji watatu walioingia fainali kwa ajili ya tuzo hiyo itakayotolewa mwezi huu.
Shirikisho la Soka Afrika (CAF) lilipunguza majina ya wanaoiwania tuzo hiyo 2013 kutoka 10, huku Toure akibaki na wachezaji 'wachovu' Didier Drogba (Ivory Coast) na John Obi Mikel (Nigeria/ Chelsea).
Jopo la makocha wa timu za taifa kutoka nchi 54 za Afrika litaamua mshindi, ambaye atatajwa katika hafla itakayofanyika mjini Lagos Januari 9.
Miongoni mwa waliokatwa katika orodha hiyo ni Mohamed Aboutrika, kiungo veterani wa Misri, ambaye Novemba aliiongoza klabu yake ya Al Ahli kutwaa taji la tano la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ndani ya miaka kumi iliyopita.
Mwingine aliyekatwa ni Jonathan Pitroipa, nyota wa timu ya taifa ya Burkina Faso ambayo iliukosa ubingwa wa Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini mwanzoni mwa mwaka na kwenye kampeni za kufuzu kwa Kombe la Dunia.
Wote hao walitarajiwa kuwa washindani wa karibu zaidi wa Yaya Toure, ambaye anapewa nafasi kubwa kushinda kutokana na mafanikio binafsi katika mwaka ambao hapakuwa na wachezaji waliokuwa na mafanikio binafsi.
Toure aliisaidia Ivory Coast kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia na amerejea kuwa nguzo muhimu katika kikosi cha klabu yake ya Manchester City ya Ligi Kuu ya England.
Kama atafanikiwa kuitwaa tuzo hiyo, kiungo huyo atakuwa mchezaji wa tatu kuitwaa tuzo hiyo mara tatu mfululizo, akiwafikia Abedi Pele wa Ghana aliyeitwaa kuanzia 1991-93 na Samuel Eto'o kuanzia 2003 hadi 2005.
Mikel, ambaye anasota benchi katika klabu yake ya Chelsea, ametajwa kutokana na mchango wake katika kuisaidia Nigeria kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia na kutwaa ubingwa wa Mataifa ya Afrika mwanzoni mwa 2013.
Drogba ni mshindi mara mbili wa tuzo hiyo lakini straika huyo wa Galatasaray ameshangaza wengi kutajwa katika orodha ya walioingia fainali mwaka huu baada ya mwaka ambao alitemwa katika timu yake ya taifa ya Ivory Coast.

No comments:

Post a Comment