STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 16, 2013

Uchaguzi wa TFF wapigwa 'dochi' sasa kufanyika Okt 27

Na Boniface Wambura
UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF uliokuwa umepangwa siku moja na pambano la watani wa jadi Simba na Yanga, sasa umesogezwa mbele kwa wiki moja na sasa utafanyika Oktoba 26 na 27 mwa huu.
Maamuzi ya kusogezwa mbele kwa uchaguzi huo ambao tangu Desemba mwaka jana umekuwa ukipigwa danadana yaliyotolewa naKamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuzingatia mamlaka iliyonayo katika kifungu cha 10(6) cha Kanuni za Uchaguzi za TFF na kuusogeza mbele hadi tarehe hiyo mpya.
Sababu za kusogeza mbele uchaguzi ni kutokana na ukweli kuwa Oktoba 20 mwaka huu uongozi wa TFF utakuwa na shughuli nyingi za maandalizi ya mechi ya Simba na Yanga, na hivyo haitawezekana kusimamia shughuli za Mkutano Mkuu wa Uchaguzi kwa wakati mmoja na mchezo huo.
Siku ya mwisho ya kampeni itakuwa Oktoba 25 mwaka huu. Ukiondoa  mabadiliko hayo ya tarehe ya uchaguzi wa viongozi wa TFF, ratiba ya mchakato wa uchaguzi na itabaki kama ilivyotangazwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF katika mkutano wake na waandishi wa habari Agosti 24 mwaka huu.
Pia Kamati imeamua kuwa uchaguzi wa Bodi ya Ligi utabakia kuwa Oktoba 18 mwaka huu kama ilivyopangwa awali.
Kamati imesema inaamini wahusika wote watapokea vizuri mabadiliko hayo na inasikitika kwa usumbufu utakaosababishwa na mabadiliko hayo.

No comments:

Post a Comment