STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 16, 2013

Waislam waitana Dar kuhusiana kupigwa risasi, kukimbizwa Segerea akiwa mgonjwa kwa Sheikh Ponda


SIKU moja tu baada ya jeshi la Polisi 'kumtorosha' kininja Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania akiwa bado akiuguza jehara la kupigwa risasi alipokuwa amelazwa Hospitali ya Muhimbili (MOI), Waislam wameitana kwa ajili ya kutoa tamko na kuamua la kufanya kutokana na kadhia hiyo.
Sheikh Ponda anadaiwa kupigwa risasi na Polisi mkoani Morogoro mara baada ya kumaliza kuzungumza na Waislam katika Kongamano la Wahadhiri wa Kiislam mkoani humo kwa kilichoelezwa kwamba anasakwa kwa kauli za kichochezi visiwani Zanzibar, ambapo awali Polisi waliruka kuwepo kwa tukio hilo kabla ya baada ya kudai ililazimika kupiga mabomu ya machozi na risasi baridi baada ya kuzuiwa na wafuasi wa Ponda wasimkamate Sheikh wao.
Sheikh huyo alipata huduma ya kwanza mjini humo kabla ya kuletwa Muhimbili, ambapo Polisi walitangaza kumtia mbaroni kisha juzi kusomewa mashtaka akiwa kitandani kabla ya jana kuondolewa kinyemela akiwa bado mgonjwa na kuifanya familia kuiachia Jumuiya ya Kiislam kuamua la kufanya.
Hivyo Waislam kupitia Jumuiya hiyo wameitisha kongamano kubwa litakalofanyika siku ya Jumapili kwenye viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke jijini Dar es Salaam ambapo kutakuwa na ajenda moja tu isemayo 'KWANINI SERIKALI YA CCM IMEMPIGA RISASI SHEIKH PONDA?'
Kongamano hilo pia linatarajiwa kufichua mambo mengine kadhaa dhidi ya dhuluma wanazofanyiwa Waislam wa Tanzania kabla ya kufanyika maandamano makubwa jijini Dar es Salaam na mikoani kupigwa udhalili wanaodaiwa kufanyiwa na serikali ya CCM.
Kwa mujibu wa vipeperushi vilivyosambazwa karibu msikiti yote mikubwa jijini Dar na hasa ile ya harakati imesema kongamano hilo litafanyika kuanzia saa 8 mchana na kuwahimiza waislam popote walipo kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kutoa maamuzi mazito yasiyotarajiwa kwa kilichoelezwa kuchoshwa na unyonge.
Kipeperushi hicho kinasema kuwa Waislam watajitahidi kupambana na hali hiyo ya unyonge kwa gharama yoyote ili amani ya kweli iweze kupatikana.
"Polisi waliotaka kumuua Sheikh Ponda, sasa wanamteka toka Muhimbili hadi Segerea akiwa bado mgonjwa, ili mfumo wa kuwakandamiza Waislam na kuwapendelea Wakristo (Mfumo Kristo) uweze kudumu na waweze kuikalia Zanzibar kinyume na matakwa ya Wazanzibar" Sehemu ya Kipeperushi hicho kinasomeka hivyo.
"Kwamba Wakristo waendelee kupoewa fedha na serikali chini ya Mkataba (MoU), wanedelee kupendelewa Baraza la Mitihani, Waendelee kupata nafasi nyingi za ajira na utawala serikalini, waendelee kuwafanya wasilam kuwa Raia wa daraja la pili, waendelee kuwazuia Waislam kutekeleza dini yao na kuwabana wasijiendeleze, ili waendelee kuwaweka Masheikh magerezani bila ya Haki. Shime Waislam"
Kipeperushi hicho kinaongeza kikionyesha kimetolewa na Jumuiya na Taasisi za Kiislam Tanzania ambalo Sheikh Ponda Issa Ponda ndiye kiongozi wake.
Katika Wahubiri wa Kiislam wametahadharisha serikali kwa kudai kuwa hata kama itaamua kumdhuru Sheikh Ponda na 'kutowesha' kabisa bado haiwezi kuwarudisha nyuma Waislam kudai haki zao kna kudai njia ya kufanya waislam watulie ni kupewa haki zao na kutendewa usawa kama wenzao wa dini nyingine.
Khatibu aliyehutubia swala ya Ijumaa msikiti Mwenge mchana wa leo, alisema waislam hawawezi kunyamaza kwa kukamatiwa au kudhuriwa kwa viongozi wao kwa madai kuwa Uislam ni dini iliyokamilika na inayoongozwa kwa mujibu wa Qur'an na mafgundisho ya Mtume Muhammad (SAW).
"Yu wapi Mtume na kipenzi cha Mwenyezi Mungu (SW), kuondoka kwake kumeuzima uislam> Hapana, makhalifa na maulamaa wangapi wamepita na uislam umebaki hivyo hivyo na nguvu zake, hivyo hata Ponda akiuwawa na masheikh wengine watafutiliwa mbali bado haiwezi kuuzima Uislam na kuwanyamzisha waislam kulilia na kutetea haki zao," alisema Khatibu huyo.
"Jambo la muhimu kwa serikali itambue na tunajua mpo vibaraka wake humu ndani nendeni mkawaambie mabosi wenu kuwa waislam HATUTANYAMAZA KUDAI HAKI ZETU mpaka iache DHULUMA kwa WAISLAM na UPENDELEO kwa WAKRISTO," alisisitiza.
Kipeperushi cha kongamano hilo la Jumapili litakalofanyika Viwanja vya Mwemba Yanga ni hiki hapa:

No comments:

Post a Comment