STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 17, 2013

Azam, Yanga hatumwi mtoto dukani! Zawania Ngao ya Hisani

Mashabiki wa Yanga watashangilia kama hivi leo mbele ya Azam

Mashabiki wa Azam watapuliza kwa mbwembwe 'kidedea' chao leo kwa Yanga?
WAKATI Yanga ikitamba itawatia adabu Azam katika pambano lao la Ngao ya Hisani linalochezwa leo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wapinzani wao hao wamesema watautumia mchezo huo kama dira na muelekeo ya timu yao kwa msimu mpya wa 2013-2014 wakipania kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza.
Meneja wa Azam, Jemedari Said alisema watashuka dimbani leo kwa tahadhari kubwa kwa kutambua kuwa huo ndiyo mchezo wao wa mwisho kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo wamepania kutwaa taji lake na wanataka kuonyesha matunda ya ziara ya kambi yao ya mazoezi nchini Afrika Kusini.
Said, alisema wanafahamu Yanga ni timu kubwa na imekuwa na upinzani mkubwa kila ikikutana na timu yao, lakini bado hawana hofu kwa sababu malengo yao makuu yapo kwenye Ligi Kuu, hivyo wanataka kuutumia mchezo huo kujua muelekeo wao kwa msimu huu.
Meneja huyo aliongeza kitu cha kufurahisha ni kwamba kikosi chao chote kilichoenda Afrika Kusini kipo fiti kikiwa hakina majeruhi wala mgonjwa, huku nyota wa wawili wa kimataifa, Brian Umony na Humphrey Mieno wameanza kufanya mazoezi mepesi ya gym kuonyesha wanaendelea vyema na majeraha waliyokuwa nayo.
"Mechi ya Ngao ya Hisani kwetu ni kipimo cha kujua tutakuwa na msimu gani safari hii, tutashuka dimbani kwa tahadhari kubwa lengo likiwa kutaka kuwoanyesha mashabiki kile tulichovuna Afrika Kusini na katika mechi zetu nane za maandalizi ya ligi zikiwemo nne za nchini humo," alisema Said.
Alisema akili yao kwa dhati kabisa ipo kwenue ligi na hasa pambano lao la ufunguzi dhidi ya Mtibwa Sugar ambalo litachezwa ugenini na mechi nyingine zijazo wakikusudia kufanya kweli na kuweka rekodi ya kutwaa ubingwa huo kwa mara ya kwanza baada ya kuhiodhiwa mfululizo kwa kupokezana kati ya Simba na Yanga.
Upande wa Yanga inayonolewa na Mholanzi, Ernie Brands, imesema haina mchecheto na pambano hilo la leo kwa vile vijana wao wapo kamili kuendeleza rekodi ya ushindi mfululizo kwa siku za karuibuni.
Kocha Msaidizi wa Yanga, Fred Felix Minziro, alisema kikosi chao kipo tayari kwa 'vita' na kwamba wangependa kutoa dozi kwa Azam kabla ya kuanza kuzishughulikia timu nyingine katika Ligi Kuu inayoanza wiki ijayo.
Yanga imepata matokeo ya ushindi katika mechi tatu mfululizo, ikizilaza Mtibwa Sugar kwa mabao 3-1 kabla ya kuinyoa 3 Pillars ya Nigeria kwa bao 1-0 na kuisulubu SC Villa ya Uganda kwa mabao 4-1 katika mechi za kirafiki za kimataifa zilizochezwa uwanja wa Taifa siku chache iliponusurika kipigo na kupata sare ya 2-2 na URA-Uganda.

No comments:

Post a Comment