STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 17, 2013

Tanzania yazidi kuchafuka duniani kisha biashara ya dawa za kulevya, mwingine anaswa Hongkong

Vitu vinadodaiwa kuwa 'unga' ukiwa umefichwa kwenye mashine
KWA mara nyingine Tanzania imeendelea kucahfuka mbele ya uso wa dunia kutokana na raia wake kujihusisha na dawa za kulevya, baada ya Mbongo mwingine kunaswa na  maafisa wa Hong Kong katika kiwanja cha ndege  akiingiza 'unga' aliouficha kwenye chuma cha mashine alichokuwa akisafiri nacho kutokea Tanzania.
 
Dawa hizo aina ya heroin zilikamatwa katika nyakati mbili tofauti kwa jumla zikiwa na kilo 1.5 na thamani ya dola milioni 1.3 za Marekani.

Maafisa hao wanasema kwa kuwa wamekuwa wakifuatilia kwa karibu nyendo za wauza dawa na mbinu za kuficha dawa hizo, walilazimika kukikata chuma cha mashine hiyo ili kuziona.

Adhabu ya kupatikana na dawa za kulevya huko Hong Kong ni faini ya dola milioni 5 za Kimarekani.

Taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya Serikali ya nchi hiyo na picha zinazoambatana na taarifa hiyo vimepachikwa hapo chini. 





No comments:

Post a Comment