STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 6, 2013

Chelsea yaifumua Norwich City, Swansea wakifa ugenini


Mshikemshike wa pambano la Chelsea na Norwich City

Chelsea
Chelsea wakipogezana baada ya kuwatungua Norwich

VIJANA wa Jose Mourinho, Chelsea jioni hii wameifumua bila huruma Norwich City baada ya kuitandika mabao 3-1, huku Swansea City ikifa ugenini kwa kulazwa na Southampton ambayo imeendeleza rekodi ya nzuri ya katika Ligi Kuu ya England.
Bao la mapema la Oscar katika dakika ya 5 na mengine ya dakika za lala salama kupitia kwa Hazard na  William yalimpa faraja Mourinho kwa kuvuna pointi muhimu tatu.
Wenyeji walipata bao lao lililokuwa la kusawazisha katika dakika ya 68  kupitia kwa Pilkington ambalo lilionekana kama lingefanya matokeo kusaliwa bao 1-1 kabla ya Chelsea kucharuka na kupata mabao mawili dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika.
Katika mechi nyingine Southampton imeendeleza libeneke kwa kuizamisha Swansea waliowafuata kwa mabao 2-0 na kuinga kwenye Nne Bora ya msimamo wa Ligi hiyo ingawa kuna mechi mbili kwa sasa zinaendelea kuchezwa zinazoweza kubadilisha msimamo ulivyo.

No comments:

Post a Comment