STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 28, 2016

Spurs yakimbilia Wembley kwa Uefa Champion League ijayo

https://static.guim.co.uk/sys-images/Sport/Pix/columnists/2015/1/28/1422488355275/tottenham-010.jpgKLABU YA Tottenham Hotspur imetangaza kuwa itacheza mechi zake za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani kwenye Uwanja wa Wembley.
Spurs ipo katika maandalizi ya kuukarabati Uwanja wao wa White Hart Lane, hivyo imeona ni vema mechi zake za UEFA ikacheza. katika Uwanja huo wa Taifa wa Uingereza wa Wembley.
Timu hiyo iliyomaliza Ligi Kuu ya England msimu huu kwa kushika nafasi ya tatu imethibitisha taarifa hizo leo Jumamosi kwa sababu ya upishaji wa matengenezo na upanuzi wa uwanja wao.

Chama cha Soka cha Uingereza (FA) kimewapa ofa pia timu hiyo kucheza mechi zao zote za Ligi Kuu za nyumbani na na zile michuano mingine ya makombe ya Uingereza kwenye Uwanja huo wa maarufu wa Wembley.

No comments:

Post a Comment