STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, May 28, 2016

'Juventus? Hapana Dani Alves hajasaini bhana!'

http://static.pulse.ng/img/football/origs4099488/8810481433-w980-h640/danialves-cropped-nghtlocydwb61j2jec4boxnqp.jpgWAKALA wa beki kisiki wa Barcelona, Dani Alves amekanusha taarifa kuwa mteja wake amesaini mkataba wa awali na Juventus, japo amekiri kuwa mabingwa hao wa Italia na klabu nyingine zinamwinda mchezaji huyo. 
Vyombo vya habari nchini Hispania viliripoti juzi kuwa beki huyo wa Barcelona anatarajiwa kuondoka baada ya kutimukia timu hiyo kwa miaka nane na kwenda Turin kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Hata hivyo, wakala wake ambaye pia amewahi kuwa mke wake, Dinorah Santa Ana da Silva alikanusha taarifa hizo akidai hazina ukweli wowote. 
Dinorah aliongeza kuwa hakuna klabu yoyote ambayo Alves aliyosaini nayo mpaka sasa kwani amehamishia nguvu zake zote katika timu ya taifa ya Brazil ambayo inakabiliwa na michuano ya Copa America inayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao. 
Wakala huyo aliendelea kudokeza kuwa, ni kweli amekutana na Juventus lakini sio wao peke yao bali ameshakutana pia na klabu nyingine, ila hakuna dili lolote lililoafikiwa mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment