STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 21, 2014

Golden Bush, Pugu Veterani kuonyeshana kazi kesho

Wazee wa 'dozi' Golden Bush Veterani
BAADA ya kimya cha muda mrefu, wakali wa soka la maveterani, Golden Bush kesho inatarajiwa kushuka dimba la Kines majira ya asubuhi kuvaana na wazee wenzao, Pugu Veterani katika mchezo wa kirafiki.
Golden Bush ambayo imekuwa ikiwasasambua wapinzani wao kwa vipigo kikubwa, mechi hiyo ya kesho dhidi ya Pugu ni kama marudiano kwani walishakutana mwishoni mwa mwaka jana na mchezo kushindwa kumalizika kutokana na kugotokea fujo, huku Pugu wakiwa wamepigwa kimoja.
Kwa mujibu wa Msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' katika pambano hilo wanatarajia kuwashikisha adabu wapinzani wao.
Ebu soma tambo wa wakali hao hapo chini mwenyewe;
Hi Wadau
 
Kwa muda mrefu kidogo nimekuwa kimya kwasababu ya majukumu ya kila siku ambayo kwa namna moja ama nyingine ilikuwa taabu kupata nafasi ya kuto matokeo huku ukizingatia kwamba timu yetu sasa hivi imekuwa ikitoa vipigo vya goli kuanzia 5 kwenda mbele. Ukipona sana 4.
 
Kesho vijana watukutu kutoka Pugu wakiongozwa machezaji mwenye maneno mengi Sele Thomas watakuwa wageni wetu katika uwanja wa St James Park, ikumbukwe game ya mwisho tuliwafunga goli moja lakini mpira uliisha dakika ya 88 pale walipoanzisha vurugu na kutuharibia game yetu. Kesho tumejipanga umpya ili kuhakikisha tunawakoma kwa kuwapa goli nyingi kama wenzao wa Stakishari walipigwa 6, Kigogo fresh 5, Mtongani 9, Mwanyamala 5 na wengine ambao siwakumbuki lakini wek kwenye akili yako kuwa walifungwa sichini ya goli 4 au 5.
 
Baada ya game hiyo huenda tukawapata ndugu zetu ambao tumewatafuta kwa muda mrefu sana, Survey Veterans siku ya jumapili inayofuata. Game hii itakuwa na umuhimi wa pekee kabisa kwasababu tunataka tuwapige goli za mwaka mzima ili wakikataa kucheza tunakuwa na hakiba ya ushindi kibindoni, hawa jamaa nina hamu nao Survey! We acha tu.
Njooni wewe, mjomba wako na shangazi yako uone football ya kesho kuanzia saa mbili kamili asubuhi

No comments:

Post a Comment