STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, January 21, 2015

Jamie Carragher awaponda wachezaji Arsenal

http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/1/photos/602000/620x/42602.jpg
Jamie Carragher
BEKI wa zamani wa klabu ya Liverpool, Jamie Carragher amewakosoa wachezaji wa Arsenal kwa kushangilia kwao baada ya kuichapa Manchester City kwa mabao 2-0 katika Uwanja wa Etihad Jumapili iliyopita.
Mabao yaliyofungwa na Santi Cazorla na Olivier Giroud yalitosha kuwapa Arsenal ushindi dhidi ya mabingwa hao wa Ligi Kuu kikiwa ni kipigo cha kwanza katika mechi 12 walizocheza.
Baada ya mchezo huo Aaron Ramsey na Alex Oxlade-Chamberlain wote walituma picha zikiwaonyesha wakishangilia katika mitandao ya kijamii jambo ambalo halijamfurahisha Carragher.
Carragher amesema haikatazwi kushangilia lakini sio timu nzima kama walivyofanya wakati hakuna taji lolote waliloshinda mpaka sasa hivyo anadhani wanapaswa kuacha.
 Carragher pia alishangazwa na aina ya mchezo uliotumiwa na meneja Arsene Wenger katika mchezo huo kwani alikuwa akizuia zaidi jambo ambalo sio kawaida yake kwani amezoea mchezo wa wazi.

No comments:

Post a Comment