STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 20, 2015

Kavumbagu wairejesha Azam kileleni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdDjGKemN2sVnPU1l723rHo-UtuVjBZ673i-L4ZgSmKzLiH8dPrkov8VclFd1qQYP1c48z_omeSmeZFlSwvlBweJ0Ous2ja2z3bmlzGANL_dA-GQmz780dcej0AwtKL-Z13vKA-TDyjsQ/s1600/HERM5672-1.JPG
Kikosi cha Azam
MABAO mawili kutoka kwa Mrundi, Didier Kavumbagu na jingine la Kipre Tchetche, limeiwezesha Azam kurejea kileleni katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara naada yua kutungua Kagera Sugar mabo 3-1.
Pambano hilo la kiporo lilichezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, na iliowachukua Azam dakika tatu kuandika bao kupitia kwa Kipre Tchetche kabla ya Kavumbangu kufunga bao la pili.
Kagera walipunguza idadi ya magoli kipindi cha pili kutipia Rashid Mandawa, lakini Kavumbagu alirejea tena nyavuni kuandika bao la tatu na lililokuwa la saba kwake msimu huu na kuipa ushindi muhimu mabingwa watetezi hao walifikisha pointi 20 baada ya mechi 10.
Azam imeiengua Mtibwa Sugar wenye pointi 17, ingawa wakata miwa hao wa Manungu wana mchezo mmoja mkononi na Jumamosi wanatarajiwa kuvaana na Ruvu Shooting uwanja wa Mabatini, wakati Azam watakuwa na kibarua kigumu jijini Dar dhidi ya Simba waliorejea upya kwenye ligi hiyo chini ya kocha Goran Kopunovic.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Mtibwa Sugar     09  04  05  00  12  05  07   17
02. Azam                 10  06  02  02  14  07  07   20
03. JKT Ruvu           11  05  02  04   11   10  01  17
04. Yanga                09  04  03  02  11   07  04  15
05. Polisi Moro         11  03  06  02   09  08  01  15
06. Kagera Sugar     11  03  05  03   08  08  00  14
07. Coastal Union     10  03  04  03   09  08  01  13
08. Mgambo JKT       10  04  01  05   05  09  -4  13
09. Simba                09  02  06   01   09   07  02  12
10. Ruvu Shooting    11  03  03   05   05   08  -3  12
11. Mbeya City         09   03  02   04  04   06  -2   11
12. Stand Utd           11  02  05   04   07   13  -6  11
13. Ndanda Fc          11  03  01   07  10    16  -6  10
14. Prisons               10  01  05   04  06   08  -2   08
Wafungaji:
7- Didier Kavumbagu(Azam)
5- Ame Ali (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)
3-
Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba),  Jacob Massawe (Ndanda)

Ratiba ya mechi zijazo

Jan 24, 2015 
Azam vs Simba 
Kagera Sugar vs Ndanda
Stand Utd vs Coastal Union 

Polisi Moro vs Yanga

Mbeya City vs Prisons
Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar 

Jan 25, 2015JKT Ruvu vs Mgambo JKT

No comments:

Post a Comment