STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, January 20, 2015

Louis Van Gal awacharukia mashabiki Man Utd

http://www.oslobodjenje.ba/portal/images/articles/louis-van-gaal-od-srijede-novi-trener-manchester-uniteda_1399028363.jpg
Kocha Louis Van Gaal
KOCHA wa klabu ya Manchester United, Louis Van Gaal amesisitiza kuwa hakubadili mfumo wa kiuchezaji katika mchezo dhidi ya Queens park Rangers kutokana na malalamiko ya mashabiki.
Mashetani Wekundu hao walianza na mfumo wa kuchezesha mabeki watatu nyuma ilishindwa kuonyesha makeke mpaka walipobadilisha na kuanza kucheza 4-4-2 baada ya mashabiki kupaza sauti zao kutoka jukwaani ndipo matunda yalipoanza kuonekana.
Lakini Van Gaal amesema kubadili mfumo ilikuwa mipango yake ya kiufundi katika mchezo huo hivyo kwamba amesikiliza mashabiki walichokisema sio kweli.
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa United ina mashabiki zaidi ya milioni 600 hivyo hadhani kama ataweza kuchukua maoni ya kila mshabiki. Van Gaal amesema kazi yake ni kuangalia, kuwasiliana, kuchambua na kuona makosa yanayofanywa na wachezaji wake wakiwa uwanjani na sio kusikiliza mashabiki wanasemaje.
Mashabiki hao wa Manchester City pia walionyeshwa kushangaza na kocha wao kumcheza Angel di Maria kama mshambuliaji na Wayne Rooney kucheza kama kiungo huku beki Jonas akiachiwa kupiga mipira ya kona.

No comments:

Post a Comment