STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, January 30, 2014

Kiungo Yohan Cabaye rasmi PSG

Cabaye asaini rasmi Paris St Germain.
MABINGWA wa Ufaransa PSG, hatimaye imemsajili kiungo,Yohan Cabaye kutoka Newcastle United kwa kiasi cha pauni milioni 20.
Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 28 amesaini mkataba wa miaka mitatu na nusu kwa klabu hiyo ya Ligue 1.
Cabaye alisema kuwa”Ninafuraha sana kurejea Ufaransa,ofa kutoka kwa PSG ilikuwa ngumu sana kuikataa,nataka kushinda mataji na nina furaha kubwa kupata nafasi ya kucheza ligi ya mabingwa barani ulaya.”
Nyota huyo ambaye pia ni kiungo wa timu ya Taifa ya Ufaransa aliichezea Newcastle United jumla ya michezo 79 na kufunga goli 17.
Pia Cabaye katika kipindi cha usajili uliopita wa majira ya kiangazi,alishawahi kutaka kuiacha klabu hiyo ya Uingereza huku akilazimisha kuhamia Arsenal bila mafanikio

No comments:

Post a Comment