STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Manchester Utd yakaribia kumnasa Blind

http://completesportsnigeria.com/wp-content/uploads/2014/07/Daley-Blind.jpg
Delay Blind
KLABU ya Manchester United imekubaliana na Ajax Amsterdam ya Uholanzi kutoa kitita cha pauni millioni 13.8 kumnunua mlinzi wa timu hiyo Daley Blind.
Blind ambaye ana umri wa miaka 24 alikuwa katika kikosi cha Kombe la dunia cha Uholanzi chini ya mkufunzi Louis Van Gaal na inaelezwa amesalia kidogo kutua mikononi mwa kocha huyo anayeinoa kwa sasa Mashetani Wekundu ambao bado 'hawajatulia' katika Ligi Kuu ya England.
Blind anaweza kucheza kama beki wa kushoto na pia beki ya kati na iwapo makubaliano hayo yatatiwa sahihi, huyo atakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na klabu hiyo.
Manchester imeshatumia zaidi ya pauni millioni 130 katika msimu huu pamoja na kuvunja rekodi ya England kwa kusajili Angel Di Maria kwa kitita cha pauni 59.7 kutoa Real Madrid, pia  memnunua beki wa kushoto Luke Shaw, Marco Rojo na kiungo matata Ander Herrera.

No comments:

Post a Comment