STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Simba yairarua KMKM x5 Zenji

Tambwe akishangilia moja ya mabao yake na Ramadhani Singano 'Messi'
KLABU ya soka ya Simba imeirarua bila huruma mabingwa wa Zanzibar, KMKM kwa kuicharaza mabao 5-0 katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyochezwa usiku wa kuamkia leo visiwani humo.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Amaan,  ilishuhudia vijana wa kocha Ally Bushiri ‘Bush’ ambayo katikati ya wiki walichezea kichapo cha mabao 2-0 toka kwa Yanga ikienda mapumziko ikiwa tayari imeshashindiliwa mabao 4-0.
Simba ilipata mabao yake kupitia kwa  Amisi Tambwe aliyefuinga mawili,, Amri Kiemba, Shaaban Kisiga ‘Marlone’ na Elias Maguli.
Kiemba alianza kuifungia Simba bao dakika ya tatu ya mchezo baada ya kumalizia pasi murua ya Pierre Kwizera kabla ya Tambwe kufunga la pili dakika ya 14 na kuongeza jingine dakika  23 kabla ya Kisiga kufunga la nne dakika ya 37 na katika kipindi cha pili Maguli kuhitimisha karamu hiyo ya magoli.

No comments:

Post a Comment