STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Arsenal bado haijatulia, Sanchez aendelea kufunga

Alexis Sanchez scores his first Premier League goal for Arsenal
Sanchez akifunga bao la Arsenal
Jamie Vardy goes close to putting Leicester 2-1 in frontYaya SanogoARSENAL imeendelea kugawa pointi bada ya kulazimishwa sare ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya Engaland dhidi ya timu ya Leicester City uwanja wa ugenini.
Vijana wa Arsene Wenger walilazimisha sare ya 2-2 na Everton kabla ya leo kupata sare ya 1-1 kwa Leicester City waliotanguliwa kufungwa bao katika dakika ya 20.
Bao hilo liliwekwa kimiani na Alexis Sanchez kabla ya Leonardo Ulloa kulirejesha dakika mbili baadaye.
Kwa matokeo hayo Arsenal wameongeza kibindoni pointi moja na kufanya wafikishe tano baada ya mechi tatu na itarejea nyumbani kuisubiri mabingwa watetezi Manchester city katika mechi ya ligi hiyo wiki mbili zijazo yaani Septemba 13.
Bao la Sanchez ni la pili katika mashindano baada ya katikati ya wiki kufunga bao pekee lililoivusha Arsenal hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment