STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 29, 2014

KOZI YA UKUFUNZI WA UTAWALA YA FIFA KUFANYIKA DESEMBA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-2-gEQjN-kUTDr5XYxr2xEbeHBZeqpiBVaxDBdXtEHTCTfXJMtFnrt4_lV5Gtu_cfAfZtDPsXoHZdVtbLhyphenhyphenBQsa9f8OgTtpmurttsK_XY2cD3KZVsKqVdjpzI97j-jLPVmU6Qy3ft4BE/s1600/mwesigwa.JPG
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa aliyesimama
SHIRIKISHO la Soka Tanzania,TFF kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameandaa kozi ya ukufunzi wa utawala itakayofanyika Desemba mwaka huu.
Kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka FIFA itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 1 hadi 5 mwaka huu, ambapo sifa ya chini ya elimu kwa wanaotaka kushiriki ni kidato cha nne.
Kwa wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi yao kwa Katibu Mkuu wa TFF. 
Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 5 mwaka huu ambapo wanatakiwa pia kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya kitaaluma.

No comments:

Post a Comment