STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 9, 2016

Rodriguez azigonganisha Manchester City, United

https://metrouk2.files.wordpress.com/2014/06/875x10001.jpg
James Rodriguez

KLABU ya Manchester City imeingia kwenye vita dhidi ya mahasimu wake, Manchester United katika mbio za kumwania nyota wa Real Madrid, James Rodriguez.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia amekuwa akiwindwa pia na mabingwa wa Ufaransa, PSG, lakini duru la kispoti zinadokeza kuwa, Rodriguez ambaye kusalia kwake Santiago Bernabeu ni majaliwa anawindwa na mabingwa hao wa zamani wa England.

City chini ya kocha mpya, Pep Guardiola imevutiwa na Mfungaji Bora huyo wa Kombe la Dunia 2014 na kwamba wapo tayari kumwaga kitita ili kumnyakua.
Klabu za PSG na Bayern Munich iliyo chini ya Kocha mpya, Carlo Ancelotti aliyewahi kumnoa Rodriguez wakati akikinoa kikosi cha Blancos, nao wanatajwa kumnyemelea mkali huyo ambaye amekuwa hana raha Real Madrid kutokana na kuishia benchini.
Rodriguez ambaye ni nahodha wa Colombia kwa sasa yupo kwenye vita ya kuisaidia timu yake kufanya vema katika michuano ya Copa America 2016 inayochezwa Marekani.

No comments:

Post a Comment