STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 7, 2014

Spurs, Everton yapeta Ligi Ndogo Ulaya, 2 zikifuzu mtoano

Benjamin Stambouli (left) and Asteras' Pablo Mazza battle for the ball at the Theodoros Kolokotronis Stadium
Kizaazaa katika pambano la Spurs wakati ikishinda 2-1
Andros Townsend opened the scoring for the English side converting a penalty he won after being fouled in the box
Andors Townsend akifunga bao la kwanza la Spurs
Phil Jagielka akishangilia bao la pili la Everton
Osmond akishangilia bao la kuongoza la Everton nyumbani jana dhidi ya Lille
32min: Mind you, Osman is looking handy now as his cross results in Lukaku glancing a header just off target.
Naismith akifunga bao la tatu la Everton jana
Lukaku akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Lille
TIMU za soka za Tottenham Hotspur na Everton za England zimeendelea kutamba kwenye michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europe League) baada ya kupata ushindi katika mechi za zilizochezwa viwanja tofauti.
Everton ikiwa nyumbani Goodson Park, walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Lille ya Ufaransa katika mechi ya kundi H na kuwafanya wasaliwe pointi chache kabla ya kufuzu hatua ya mtoano.
Mabao ya washindi yaliwekwa kimiani na leon Osman katika dakika ya 27, Phil Jagielka Dk 42 na la kipindi cha la Steven Naismith.
Everton imefikisha pointi nane sawa na Wolfsburg wanaoshika nafasi ya pili nyuma yao.
Nayo Spurs ikiwa ugenini  nchini Ugiriki ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Asteras Tripolis na kuongoza kundi C.
Andors Townsand alifunga bao la kuongoza dakika ya 36 kwa mkwaju wa penati kabla ya Harry Keane kufunga bao lake la nane katika mechi nane za Spurs dakika ya 42.
Wenyeji walipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 90 huku Spurs ikimpoteza Feredico Fazio kwa mchezo mbaya.
Katika michezo mingine Dinamo Moscow ilipata ushindi wa bao 1-0 na kujihakikishia tiketi ya kucheza hatua inayofuata kwa kuilaza Estoril, huku Qarabağ ikikubali kipigo nyumbani cha mabao 2-1 dhidi ya Dnipro Dniprop.
Zürich ilishinda nyumbani mabao 3-2 dhidi ya Villarreal, Apollon ililala 2-0 nyumbani mbele ya Borussia M'gla.
HJK  nayo ilitakata kwao kwa kuilaza Torino kwa mabao 2-1, huku    København ilifumuliwa kwao kwa mabao 4-0 na Club Brugge wakati
Beşiktas ilishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Partizan.
Mechi nyingine zilishuhudia Astra na Celtic zikitoshana nguvu kw akufungana bao 1-1,         Dinamo Zagreb ikilala kwao kwa mabao 5-1 mbele ya Salzburg na     Panathinaikos ikafungwa mabao 3-2 na PSV.
Timu ya Saint-Étienne na Inter Milan zilifungana bao 1-1, huku Feyenoord ikiitambia wageni wao Rijeka kwa mabao 2-0, Sevilla ikiwa nyumbani ikailaza Standard Liège mabao 3-1 na
Wolfsburg ikaicharaza Krasnodar kwa mabao 5-1 na Sparta Prague ikaicharaza Slovan Bratislava kwa mabao 4-0.
Napoli ya Italia ikiwa nyumbani iliitambia Young Boys kwa mabao 3-0 na  Dynamo Kiev     ikashinda nyumbani kwa mabao 2-0 dhidi ya AaB, nayo Rio Ave na Steaua Bucharest zilitoka sare ya 2-2, Guingamp ikashinda 2-0 dhidi ya Dinamo Minsk, huku Fiorentina na PAOK zikifungana bao 1-1 kama ilivyokuwa kwa timu za Lokeren na Trabzonspor, huku Legia Warszawa     iliifunga mabao 2-1 Metalist.

No comments:

Post a Comment