STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Breaking News! Mwanamuziki Khamis Amigolas afariki dunia

http://api.ning.com/files/dyEc5o4i5R40CVU*duc5GvfEdRdfsq*YNDQExCkCTTWwBhKlKRvwR7nmiRAkRIilv-ILlXQzgl*2lrXVs1ybGjHfMVry78iT/amigo2.jpg?width=450
Amigolas enzi za uhai wake
MWANAMUZIKI nyota wa zamani wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Khamis Kayumbu 'Amigolas'  amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Muimbaji huyo aliyekuwa bendi ya Ruvu Star, amekumbwa na mauti hayo baada ya kulazwa hospitalini hapo kwa tatizo la Moyo kwa siku kadhaa.
Muasisi huyo wa Twanga Pepeta na anayekumbukwa na utunzi mahiri wa wimbo wa Aminata, alilazwa hospitalini hapo wiki mbili zilizopita na alikuwa katika maandalizi ya kufanyiwa upasuaji juu ya tatizo lake.
Mpaka anafariki mkali huyo ndiye aliyekuwa kiongozi wa bendi ya Ruvu Star ambayo inatamba na nyimbo zake tatu za awali na walikuwa wakijiandaa kumalizia nyingine mbili kabla ya kzuindua albamu yao ya kwanza.
Kabla ya kuzipigia Twanga Pepeta na Ruvu Stars, marehemu Amigolas enzi za uhai wake alifanya kazi na bendi za Bicco Stars chini ya Kinguti System.
Msiba uko nyumbani kwa mama mzazi wa marehemu Mburahati jijini Dar es Salaam jirani kabisa na Shule ya Msingi Mianzini, na kwamba taratibu za mazishi zinasubiri ndugu na jamaa kutoka Tabora na Kigoma.


No comments:

Post a Comment