STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Spurs yapigwa tena, Newcastle yatakata, Everton droo

Bojan
Stoke wakishangilia mabao yao dhidi ya Spurs
Ayoze Perez, Newcastle
Newcastle United iliyoitambia WBA nyumbani kwao
Leighton Baines
Everton wakifunga bao lao dhidi ya Sunderland
WAKATI Tottenham Hotspur ikiendelea kutoa takrima nyumbani kwake kwa kuruhusu kipigo kingine toka kwa Stoke City kwa kulazwa mabao 2-1, Newcastle United imeendelea na maajabu yake baada ya kupata ushindi ugenini dhidi ya West Bromwich Albion katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Newcastle ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji wao kupitia kwa Ayoze Perez aliyefunga dakika ya 45 kabla ya Fabricio Coloccini aliyemaliza udhia katika dakika ya 62.
Spurs ambayo imekuwa ikifanya vyema kwenye Ligi Ndogo ya Ulaya, ilikumbana na kipigo kingine cha aibu nyumbani uwanja wa White Hartlane kutoka kwa Stoke City.
Wageni waliandika bao la kuongoza dakika ya 6 kupitia Bojan kabla ya Jonathan Walters kuongeza la p[ili dakika ya 33 na Spurs kupata la kufutia machozi kipindi cha pili katika dakika ya 77 kupitia Nacer Chadli, ksiha wenyeji kumpoteza beki wake Naughton kwa kucheza madhambi dhidi ya Victor Moses.
Katika pambano jingine la ligi Everton imejikuta iking'ang'aniwa ugenini na Sunderland kwa kulazimishwa sare ya 1-1.
Pambano linaloendelea sasa ni Arsenal ikiwa ugenini inaumana na Swansea City

No comments:

Post a Comment