STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Juventus yaiangamiza Parma 7-0 Italia

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Stephan+Lichtsteiner+Juventus+v+Parma+FC+Serie+wN6nAJVItT9l.jpgMABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Serie A, Juventus imeifanyia mauaji ya kutisha timu ya Parma kwa kuicharaza mabao 7-0 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Juve wakiwa uwanja wa nyumbani walipata ushindi huo kupitia mabao yaliwekwa kimiani na Llorente, Carlos Tevez na Alvaro Morata waliofunga mawili kila mmoja na jingine la Stephan Lichtsteiner.
Llorente alianza kuandika bao dakika ya 23 kabla ya Lichtsteiner kuongeza la pili dakika ya 29 na Llorente kurudi tena dimbani kwa kufunga bao la tatu katia dakika ya 36.
Carlos Tevez alifunga mabao mawili ndani ya dakika nane katika dakika ya 50 na 58 kabla ya Álvaro Morata kumalizia kazi katika dakika ya  76 na 88.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Cagliari na Genoa zilitoshana nguvu kwa kufunga bao 1-1, huku Chievo Verona ikipata ushindi nyumbani dhidi ya Cesema kwa kuilaza mabaop 2-1, Empoli ikainyoa Lazio pia mabao 2-1 na Palermo ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Udinese.

No comments:

Post a Comment