STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Borussia Dortmund yapumua kwa bao la 'kupewa'

Christoph Kramer
Safi sana! Wachezaji wa Borussia wakimpa pole Kramer baada ya kujifunga bao lililowapa pointi tatu muhimu
BAO pekee la kujifunga la Borussia Monchengladbach la dakika ya 58 liliwapa ushindi muhimu timu ya Borussia Dortmund katika mechi ya Ligi ya Ujerumani Bundesliga.
Christoph Kramer alijifunga bao wakati akirudisha pasi ya nyuma kwa kipa wake Yann Sommer na kuifanya Dortmund iliyokuwa mkiani kuchupa hjadoi nafasi ya 15 kwa kufikisha pointi 10.
Wapinzani wao wamesaliwa kwenye nafasi ya tatu nyuma ya timu za Bayern Munich inayoongoza na pointi 27 na Wolfsburg walio na pointi 23 baada ya kuifunga Hamburger  kwa mabao 2-0 katika mechi nyinmgine wakati ligi ikimaliza mzunguko wa 11.

No comments:

Post a Comment