STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Mtibwa Sugar yang'ang'aniwa na Kagera, kiporo chao chaisha 1-1

Kikosi cha Mtibwa kilicholazimishwa sare ya 1-1 na 'ndugu' zao wa Kagera Sugar
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Mtibwa Sugar imeshindwa kulinda ushindi wake iliyopata katika dakika 45 za kwanza zilizochezwa juzi baada ya jana Kagera Sugar kurudisha bao na kufanya matokeo kuwa bao 1-1.
Kwa mujibu wa Msemaji wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru, dakika 45 za pili zilipigwa jana asubuhi kwenye uwnaja wa Manungu Complex, Turiani na Kagera kupata ushindi wa bao 1-0.
Bao la Kagera liliwekwa kimiani na Rashid Mandawa katika dakika ya 56 na kuwa la kusawazisha ambalo Mtibwa Sugar ilipata katika dakika 45 za kwanza zilizochezwa juzi kwenye uwanja huo kabla ya pambano kuvunjwa kwa sababu ya mvua kubwa iliyonyesha.
Katika dakika 45 za kwanza bao la Mtibwa liliwekwa kimiani na Ame Ally 'Zungu' dakika mbili kabla ya mapumziko na kumfanya mshambuliaji huyo aliyesajiliwa akitokea Chuoni ya Zanzibar kufikisha bao la nne.
Idadi hiyo imemfanya kulingana na wachezaji Didier Kavumbagu wa Azam na Danny Mrwanda wa Polisi.
Matokeo hayo yameifanya Mtibwa kwenda mapumziko nikiwa bado kileleni ikiwa na pointi 15, ikifuatiwa na Yanga na Azam zenye pointi 13 kila moja na Coastal Union ikifuatiwa na pointi zake 11.

MSIMAMO WA LIGI ULIVYO SASA:

                               P   W   D    L   F    A   GD  Pts
01. Mtibwa Sugar    07  04  03  00  10   03  07  15
02. Azam                07  04  01  02   08  04  04  13
03. Yanga               07  04  01  02  09   05  04  13
04. Coastal Union   07  03  02   02  09   07  02 11
05. Kagera Sugar   07  02  04   01  06   04  02  10
06. Polisi Moro        07  02  03  02   06   07  -1  09
07. Mgambo JKT    07  03  00  04   04   07   -3  09
08. Stand Utd         07  02  03  02   05   09  -4  09
09. JKT Ruvu         06   02  01  03   05   07  -2  07
10. Ruvu Shooting 06  02  01  03   04   06  -2  07
11. Simba              06  00  06  00   06   06  00  06
12. Prisons            07  01  03  03   06   07   -1  06
13. Ndanda Fc       06  02  00  04   08  10   -2  06
14. Mbeya City       07  01  02  04   02   06  -4  05

Wafungaji:
4-
Didier Kavumbagu(Azam), Ame Ally (Mtibwa), Danny Mrwanda (Polisi-Moro)

No comments:

Post a Comment