STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Marehemu Amigolas kuzikwa kesho makaburi ya Kisutu

Amigolas enzi za uhai wake
MWILI wa aliyekuwa kiongozi na mwanamuziki wa bendi ya Ruvu Stars aliyewahi kutamba na benchi za Bicco Stars, Chezimba Band na African Stars 'Twanga Pepeta', Khamis Kayumbu 'Amigolas' unatarajiwa kuzikwa kesho baada ya swala ya Alasir katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO muda mfupi uliopita, mmoja wa viongozi na mwanamuziki aliyefanya kazi kwa muda mrefu na Amigolas, Rogert Hegga 'Catapillar' alisema kuwa, imethibitika kuwa mwili wa mwenzao utahifadhiwa kesho saa 10 jioni kwenye makaburi ya Kisutu.
Hegga alisema awali mama wa marehemu baada ya kuwasiliana na ndugu na jamaa waliopo mikoa ya Tabora na Kigoma, ilikuwa marehemu azikwe leo, lakini kutokana na rai ya watu wengi kutokana na umaarufu aliokuwa nao Amigolas, mwili huo sasa utazikwa kesho.
"Baada ya mama wa marehemu kuzungumza na ndugu na jamaa zake waliopo Tabora na Kigoma, imeamuliwa marehemu azikwe kesho (leo) Jumatatu baada ya swala ya Alasir," alisema Hegga.
Muasisi huyo wa Twanga Pepeta aliyewahi kutamba na wimbo wa 'Aminata', alifariki usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya taifa ya Muhimbili alikolazwa kwa maradji ya Moyo.

No comments:

Post a Comment