STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Ruvu Shooting kuvunja 'ndoa' ya Simba, Phiri? JKT, Ndanda Chamazi

http://1.bp.blogspot.com/-bdeY6ALCWMw/VDApTyxy8_I/AAAAAAAAppw/mBc2LYYxgvs/s1600/HMB_8444.JPG
Simba watashangilia kama hivi au itakuwa 'majanga'
Patrick Phiri, Kocha wa Simba akizungumza na wachezaji wake
Ruvu Shooting waliotamba kuigaragaza Simba leo Taifa. Wataweza?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgjyChPvvQH5BYDde3oWaCPF7Ng3bP6-d1hrZ9FSSrbj4l6LzO1da-EXcr6HYFz0pu6qt7ApERxitRyxjUGKcWbZp6h1dp8qy-Rj9uw2wwmw4aQlTBuZgmptzQm8pKvaqeH0A5AME79rwmE/s1600/JKT+RUVU+2014.JPG
JKT Ruvu itavuna nini kwa Ndanda Fc leo Chamazi?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSvHwYqtPQMuzPoWUu4QCWVjjgvVwLySqdBYExhW-LxDkl-tjqI3X__y-_vwNzmO6A72piQEbxsK79AqJ8vub5o2bTvjx1VL8FqSFT_-uMryVYDTOmZZVv18G_WiMV4YrQE_D_be0p_aWy/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda Fc itaendeleza kipigo baada ya kuzidnuka kwa Azam?
WAKATI uongozi wa klabu yake ukikanusha taarifa za kuwa na mipango ya kumleta aliyekuwa Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen, kocha  Patrick Phiri leo atakuwa katika kibarua kizit cha kulinda ajira yake wakati wake wa Simba watakaposhuka dimbani kuwakabili Ruvu Shooting katika mechi ya mwisho kati ya mbili alizopewa na uongozi.
Uongozi wa Simba ulitangaza kumpa kocha huyo wa kimataifa kutoka Zambia mechi mbili za mwisho kabla ya kumfuta kazi kama Simba haitaweza kupata ushindi. Mechi ya kwanza ilikuwa dhidi ya Mtibwa ambayo iliisha kwa sare ya 1-1, ikiwa ni sare ya sita mfululizo kwa mabingwa hao wa zamani wa soka nchini.
Matokeo yoyote tofauti na ushindi kwa Simba leo itakuwa na maana kwamba Phiri atafungasha virago vyake kurudi kwao Zambia kwani atakuwa ameshindwa kutekeleza masharti ya mabosi wake ambao waliibuka katikati ya wiki kukanusha taarifa za kuwepo na mipango ya kumleta Kim Poulsen kuchukua nafasi ya Mzambia huyo.
Hata hivyo Phiri pamoja na vijana wake walionukuliwa wakidai kuwa wapo tayari kufutwa naye kazi kuliko kuona anaondolewa kwa sababu sare wanazopata ni sehemu ya matokeo ya mchezo, wameapa kufa na Ruvu ambayo baada ya ushindi mfululizo katika ligi hiyo ilijikuta wakizimwa na mabingwa wa zamani Coastal Union kwa kulazwa bao 1-0.
Phiri alisema hana hofu ya kutimuliwa kwani makosa yaliyowagharimu katika mechi zilizopita yamerekebishwa na leo wadau wa Msimbazi wajiandae kucheka kwa furaha ya ushindi kwa mara ya kwanza baada ya mechi 11 mfululizo.
Simba ambayo itaendelea kukosa huduma za nyota wake watatu, Shaaban Kisiga mwenye mabao mawili mpaka sasa katika orodha ya wafungaji msimu huu, Amri Kiemba na Haruna Chanongo wamesimamishwa muda usiojulikana kwa madai ya utovu wa nidhamu na kucheza chini ya kiwango.
Pia haitakuwa na kipa wao Hussein Sharrif 'Casillas' anayeuguza jehara la upasuaji wa ugoko aliofanyiwa Afrika Kusini hivi, lakini itakuwa na mkali wao kutoka Uganda, Emmanuel Okwi ambaye mpaka sasa amefunga mabao mawili.
Ruvu Shooting wenyewe kupitia Msemaji wao, Masau Bwire imekuwa ikisisitiza kuwa, Simba isitarajie mteremko na kuwa klabu ya kwanza kuwapa pointi tatu kwa sababu wamepania kuwapa kipigo ili kuurahisishia kazi uongozi juu ya azma yao ya kumtimua kocha Phiri.
"Hapa kwetu hata sare hawapati, maana tulisikia kundi la 'waasi' ndani ya klabu hiyo Ukawa kuwa Simba ingepata sare mfululizo mechi saba. Sisi ndiyo tutakaokuwa klabu ya kwanza kuwafunga Simba msimu huu. Tumepania na Simba isitarajie wepesi kwetu," alisema Bwire.
Bwire alisisitiza kipigo walichopewa na Coastal kimewazindua na kurekebisha kikosi chao ili kuendeleza wimbi la ushindi kama ilivyokuwa awali kwa kuzifunga Ndanda nyumbani kwao na baadaye Polisi Moro uwanja wa Mabatini.
Ruvu Shooting wana pointi 7 baada ya mechi sita wakishinda mbili, kutoka sare moja na kupoteza tatu wakiwa kwenye nafasi ya nane wakati wapinzani wa wakishika nafasi ya 10 wakiwa na pointi 6.
Katika mfululizo wa ligi hiyo leo pia kutakuwa na pambano jingine litakalozikutanisha timu za JKT Ruvu dhidi ya Ndanda, huku kila timu ikiwa katika hali tofauti, Ruvu ikiuguza kipigo cha Polisi-Moro na Ndanda ikichekelea kuitoa nishai Azam katika mechi zao zilizopita.

No comments:

Post a Comment