STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 9, 2014

Pacquiao kutua nchini mwakani, Mtanzania kusindikiza pigano lake Macao

http://fightnights.com/uploads/manny-pacquiao.jpg
Manny Pacquiao
BINGWA wa Dunia wa WBO uzani wa Welter, Manny Pacquiao anatarajiwa kutua nchini Februari mwakani kuja kushuhudia pambano la kimataifa la Ngumi za Kulipwa kama mgeni rasmi.
Aidha mmoja kati ya mabondia watatu wa uzani wa Feather (kilo 57) Cosmas Cheka, Sadiki Momba au Mohammed Matumla 'Snake Boy Jr' anatarajiwa kuteuliwa kwenda kupigana pambano la utangulizi wakati Pacquiao atakapokuwa akitetea taji lake dhidi ya Chris Algieri siku ya Novemba 22.
Pambano hilo la Pacquiao na Algieri litafanyika kwenye ukumbi wa Cotai Arena, Venetian Resort mjini Macoa nchini China.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania, PST, Anthony Rutta aliliambia MICHARAZO kuwa walikuwa wakifanya mazungumzo na meneja wa bingwa huyo wa dunia na mwanasiasa nchini Ufilipino aje nchini mwakani.
Rutta alisema PST kupitia Bingwa wa zamani wa dunia wa uzito wa juu wa WBF,  Francois Botha aliyekuja nchini wakati wa pambano la Francis Cheka dhidi ya Mmarekani, Phil Williams wanafanya mazungumzo ili bondia huyo kuja nchini.
"PST inafanya mpango wa kumleta Manny Pacquiao nchini Februari kuja kuwa mgeni rasmi wa pambano la kimataifa kati ya bondia wa Tanzania mpinzani wa kigeni toka Ulaya," alisema Rutta.
Alisema mipango hiyo inakuja wakati PST imepata ofa ya kumpeleka bondia mmoja kucheza pambano la utangulizi wakati Pacquiao akitetea taji lake na Algieri wiki mbili zajazo.
"Tumepewa ofa kupitia Botha kutuma bondia mmoja kucheza pambano la utangulizi wakati Mfilipino huyo akitetea taji lake na hii itakuwa mara ya kwanza kwa bondia wa Tanzania kushindikiza pambano kubwa kama hilo," alisema.
Alisema kwa sasa wanafanya mchakato wa kuteua bondia mmoja kati ya watatu wenye sifa na kilo ziliotakiwa kati ya Momba, Matumla na Cheka mdogo.
"Mmoja kati ya mabondia hao atateuliwa kwenda Macao kupigana, hii ni fursa ya kipekee kwa mabondia wa Tanzania," alisema Rutta.

No comments:

Post a Comment