STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 30, 2013

Mrembo Miss Utalii Tanzania kupaa kesho kwenda Equatorial Guinea

Miss Utalii Tanzania 2013

MREMBO wa Miss Utalii Tanzania 2013, Khadija Mswaga anatarajiwa kuondoka nchini kesho kuelekea Equatorial Guinea kwa ajili ya kuiwakilisha nchi katika mashindano ya kusaka mrembo wa Utalii Duniani 'Miss Tourism World 2013'.
Shindano hilo la urembo la dunia litafanyika katika nchi ya Equatorial Guinea ambapo warembo wa nchi 126 wanatarajiwa kuchuana kuwania taji hilo.
Rais wa Bodi ya Miss Utalii Tanzania, Gideon Chipungahelo 'Chipps' aliiambia MICHARAZO kuwa mrembo huyo wa Tanzania ataondoka kesho Jumanne kwa ndege ya kampuni ya Ethiopia kuelekea nchini humo tayari kwa kinyang'anyiro kitakachofanyika Oktoba 12.
Chipungahelo alisema mwakilishi wao anaenda katika shindano hilo akiwa amebeba ujumbe wa kutangaza hifadhi ya taifa ya Ngorongoro Crater kama moja ya maajabu ya dunia Afrika.
Mrembo huyo alisema ameamua kubeba ujumbe huo kwa sababu ni hifadhi ya kipekee duniani ambayo pia inaelezewa ndiyo chimbuko la binadamu wa kwanza na sehemu pekee binadamu anaishi na wanyama kwa ushirikiano bila kudhuriana.
Mrembo huyo alisema ana imani kubwa ya kufanya vizuri katika shindano hilo ili kuifuta machozi Tanzania ambayo imekuwa na bahati mbaya ya kufanya vibaya katika kila shindano la kimataifa inayoshiriki duniani.

No comments:

Post a Comment