STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Cheka ni nouma amzima Mashali na kutibua rekodi yake ya kutopigika


Bondia Fransic Cheka Kushoto akipambani na Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka Kushoto akimshambilia kwa makonde ya nguvu Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUTraundi ya nne Picha nawww.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' akishangilia ushindi uku akiwa amebebwa juu juu kama mkungu wa ndizi Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Cosmas Cheka kushoto akipambana na Charles Mashali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba siku ya mei mosi Cheka alishinda kwa ponti mpambano huo Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' akimsindikiza wakati wa kupigana bondia Ibrahimu Class 'King class Mawe wakati wa mpambano wake na amos mwamakula
Bondia Amos Mwamakula kushoto na Ibrahimu Class 'King Class mawe' wakisubili matokeo ambapo class alishinda kwa point Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Thomas Mashali kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Cheka katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT



Shomari kimbau akiwa na Cheka baada ya kumvisha ubingwa wa IBF Africa aliokuwa akiutetea
Kotoka kushoto ni Kocha wa mchezo wa ngumi Kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D' mdau ambaye ajajulikana jina Mtaalishaji wa mpambano kati ya Fransic Cheka Vs Thomasi Mashali Adamu Tanaka 'Tunaluza' na MC wa mpambano huo COOL p
Rashidi Mhamila 'Ngade akiwa amepozi na Bad Boy wakati wa onesho hilo



BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa, Francis Cheka usiku wa kuamkia leo ameendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia wenzake nchini baada ya kumtwanga kwa KO ya raundi ya 10 Thomas Mashali na kunyakua zawadi ya gari na kutetea taji lake la IBF-Afrika.
Cheka kwa kumpiga Mashali amefanikiwa kumvunjia rekodi mpinzani wake ya kutopigika nchini tangu ajitose kwenye ngumi hizo za kulipwa, ambapo kipigo cha jana kilikuwa cha kwanza kwake.
Mashali alikuwa na rekoidi ya kucheza mapambano 9 na kushinda nane na kutoka droo moja, lakini ukali wa ngumi za Cheka zilimfanya asalimu amri katika raundi hiyo ya 10 akiwa amebakisha mbili tu kumaliza mchezo huo uliokuwa wa raundi 12 la uzani wa Super Middle.
Ushindi huo wa Cheka umemfanya kuendeleza rekodi yake ya kuwapiga mabondia karibu wote nchini na kutowahi kupigwa katika ardhi ya Tanzania tangu mwaka 2008 akiwa amewachakaza karibu nyota wote nchini na Afrika Mashariki na Kati.
Cheka kwa kutetea taji lake sasa atapaswa kujiandaa kupambana tena na Mmalawi Chiotcha Chimwemwe aliyemtwanga kwa pointi walipoikutana katika pambano lililofanyika mjini Arusha ambapo alikuwa pia akitetea taji hilo alililotwaa kwa kumtwanga Mada Maugo, Aprili mwaka jana.

No comments:

Post a Comment