STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Kivumbi ya UEFA Ndogo ni leo, Chelsea kupenya kwa Basel

http://www.thenewstribe.com/wp-content/uploads/2013/04/Chelsea-vs-FC-Basel-1.jpg
Vita hii ya Basel na Chelsea inatarajiwa kujirtudia tena usiku wa leo kwenye UEFA League

IKIWA na faida ya ushindi wa mabao 2-1 iliyopata ugenini dhidi ya Basel ya Uswiss, Chalsea itawakaribisha wageni wao hao kwenye nusu fainali ya pili ya Ligi Ndogo ya Ulaya katika pambano litakalochezwa uwanja wa Stanford Bridge, jijini London.
Chelsea am,bayo inashuka dimbani ikiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata dhidi ya Swansea City katika Ligi Kuu ya England itahitaji ushindi au sare yeyote kuweza kufuzu fainali za michuano hiyo zitakazofanyika Mei 15.
Kocha wa Chelsea, Rafa Benitez ameweka bayana wameweka akili zao kwa ajili ya pambano hilo wakiwa na tahadhari kubwa kutokana na wapinzani wao kutotabirika akikumbukia walivyowaondoa michuanoni Tottenham katika mechi ya robo fainali.
Benitez amenukuliwa akisema watashuka dimbani wakiwa na dhamira kuu ya kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi ya leo, lakini hawaipuuzii Waswisi hao ambao wametoka kupokea kichapo cha mabao 3-0 katika mechi ya ligi ya nyumbani kwao dhidi ya Luzern Jumapili iliyopita.
Naye kocha wa Basel Murat Yakin, amedai inahitgaji miujiza kidogo kuweza kuwaondosha Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali na wao kutinga fainali.
Yakin alisema hata hivyo wachezaji wake wana ari kubwa na kujiamini kupita kiasi katika pambano hilo la leo dhidi ya kigogo kingine cha jiji la London baada ya awali kuiondosha Tottenham kwa mikwaju ya penati kufuatia kutoka sare ya mabao 4-4 katika mechi zote mbili.
Bila shaka ni suala la kusubiri kuona kama vijana wa darajani watatinga fainali ya pili mfululizo ya michuano ya Ulaya baada ya mwaka jana kucheza Ligi ya Mabingwa na kuiondosha patupu Bayern Munich waliotinga tena fainali hizo msimu huu baada ya jana kuing'oa kwa aibu Barcelona kwa mabao 7-0.
Pambano jingine la pili la nusu fainali ya marudiano usiku wa leo ni kati ya timu za Benfica na Fenerbache nchini Ureno.
Wenyeji hao walichezeas kichapo cha bao 1-0 ugenini nchini Uturuki wiki iliyopita, hivyo kuhitaji ushindi ili kuweka hai matumaini ya kucheza fainali hizo za UEFA Ndogo wiki mbili zijazo mjini Amsterdam, Uholanzi.

No comments:

Post a Comment