STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 2, 2013

Ni fainali ya Wajerumani, Barca wapigwa tena nyumbani na Bayern

Arjen Robben akionyesha manjonjo ya ushindi

Aah hii aibu bana! Kipa wa Barcelona na beki wake wakiwa hoi

Wachezaji wa Bayern Munich wakipongeza baada ya kuisasambua Barcelona nyumbani kwao jana


Kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Gardiolla aliyetua Bayern Munich akishangilia ushindi wa timu yake mpya na Franky Ribbery


BARCELONA, Hispania
BAYERN Munich walitinga katika fainali ya kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya itakayokutanisha Wajerumani watupu wakati walipoisambaratisha Barcelona 3-0 kwenye Uwanja wa Nou Camp jana na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 7-0.
Mabingwa hao wapya wa Ligi Kuu ya Ujerumani waliimaliza mechi mapema wiki iliyopita kwa ushindi wa 4-0 nchini Ujerumani na hapakuwa na namna ya kufufuka kwa Wahispania hao wakati Arjen Robben alipofunga goli la kuongoza dhidi ya kipa Victor Valdes katika dakika ya 49.
Kudhalilika kwa Barca kulikamilishwa mwishoni mwa mechi wakati Gerard Pique alipojifunga mwenyewe na Thomas Mueller, ambaye alifunga magoli mawili katika mechi yao ya kwanza, akapachika la tatu kwa kichwa.
Barca, kama Bayern ambao wanafukuzia taji la tano la Ulaya, wanategemea kipaji cha Lionel Messi, ambaye anarejea kutoka katika majeraha ya misuli ya nyuma ya paja na ambaye aliachwa benchi, lakini bila ya Mwanasoka Bora wa Dunia huyo hawakuwa na makali yoyote.
Bayern watacheza dhidi ya Borussia Dortmund katika mechi ya fainali kwenye Uwanja wa Wembley mjini London Mei 25 baada ya Dortmund kuitoa Real Madrid kwa jumla ya mabao 4-3 juzi Jumanne.

No comments:

Post a Comment