STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

AZAM NDIO MABINGWA WAPYA WA KOMBE LA MAPINDUZI 2017

PAMBANO la fainali ya Kombe la Mapinduzi 2017 limeisha kwa Azam kutwaa taji kwa mara ya tatu bila kupoteza pambano lolote wala kufungwa bao hata moja baada ya usiku huu kuichapa Simba kwa bao 1-0.
Bao pekee la Azam liliwekwa kimiani dakika ya 13 na Himid Mao 'Ninja' na kuifanya Azam kuweka rekodi ya aina yake katika michuano hiyo ikifanikiwa kuzilaza Simba na Yanga kwa hatua tofauti na kubwa kutoruhusu bao lolote katika michuano hii ya 11 iliyochezwa Uwanja wa Amaan.
Azam ilionekana tangu mapema kuibana Simba ambayo ilicharuka dakika za mwishoni mwa washambuliaji wake Juma Liuzio, Pastory Athanas na Laudit Mavugo wakikosa mabao ya wazi.

No comments:

Post a Comment