STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

Kocha Lyon anamtaka Depay hata leo hii

Depay
KOCHA wa klabu ya Olympique Lyon, Bruno Genesio amefichua kuwa straika wa Man United, Memphis Depay ni moja ya vipaumbele vyake katika usajili wa Januari.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi inaelezwa kuwa, huenda akaondoka klabu hapo mwezi juu kwenda katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Ufaransa, ingawa inadaiwa kikwazo ni dau la Pauni 13 milioni lililotajwa kutaka kulipwa na Lyon.
Mabosi wa Mashetani Wekundu wanataka kumuuza mchezaji huyo kwa Pauni milioni 15.
Hata hivyo, Kocha Genesio amefichua juu ya kumhitaji mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa kusema; "Depay ni kipaumbele changu."
"Ni mchezaji aliyekamilika kwa kila kitu na atatufaa kuziba nafasui ya (Rachid) Ghezzal, iwapo mchezaji huyo ataamua kuondoka Lyon," aliongeza Genesio.
Depay amekuwa hana nafasi ndani ya kikosi cha Kocha Jose Mourinho, huku ikielezwa 'ubishoo' ndio unaomponza, hivyo njia pekee ya kuokoa kipaji chake ni lazima apate timu ya kuichezea na Lyon inasisitiza inamtaka.

No comments:

Post a Comment