STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 12, 2017

Andre Ayew aitibulia Huddersfield akiibeba West Ham

Andre Ayew akiifungia West Ham bao la pili
 

Andre Ayew akishangilia bao lake

Obiang akishangilia bao lake 
LONDON, England
WEST Ham United usiku wa kuamkia leo walipata ushindi muhimu nyumbani baada ya kuichapa Huddersfield na kuitibulia rekodi yao ya kupototeza mchezo wowote tangu msimu huu wa Ligi Kuu England kuanza.
Straika Andre Ayew aliyetokea benchi alihusika na mabao yote mawili ya Wagonga Nyundo hao baada ya awali kumtengenezea bao Pedro Obiang katika ya 72 kabla ya mwenyewe kutumbukiza wavuni bao la pili dakika tano baadaye kwenye mchezo mkali uliopigwa Uwanja wa London.
Nyota huyo wa Ghana na mtoto wa Mwanasoka Bora wa zamani Afrika, Abedi Ayew Pele aliingia uwanjani dakika ya 64 kuchukua nafasi ya nyota wa zamani wa Manchester United, Javier Hernandez 'Chicharito' kabla ya kuibeba West iliyotoka kupoteza mechi yao dhidi ya NewCastle United waliowafumua mabao 3-0 ugenini.

No comments:

Post a Comment