STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Diamond kutangaza utalii wa ndani



MSHINDI wa tuzo tatu za muziki nchini na Balozi wa Malaria, Naseeb Abdul 'Diamond' ameingia makubaliano ya mwaka mmoja na waandaaji wa shindano la Miss Utalii Tanzania kwa nia ya kuhamasisha utalii wa ndani sambamba na kuendelezxa vita dhidi ya malaria.
Habari zilizopatikana jijini na kuthibitishwa na Rais wa Miss Utalii, Gideon Chipungahelo, zinasema lengo la kamati hiyo kumshirikisha Diamond ni kuunganisha nguvu za sanaa ya muziki na urembo wa kitalii katika kuunga mkono juhudi za serikali za kukuza sekta ya utalii na utamaduni pia vita dhidi ya ugonjwa hatari wa malaria nchini na Africa kwa jumla.
Katika makubaliano ya awali kati ya wawili hao ni kwamba Diamond atafanya ziara ndefu maalum ya uhamasishaji itakayofahamika kwa jina la Diamond Tanzania Kamwambie Tour-Malaria Inaua Utalii ni Maisha'.
Pia msanii huyo aliyengara kwenye tuzo za Kilimanjaro Music Awards-2010, atatunga kibao maalum kwa ajili ya Miss Utalii Tanzania 2010 ambao ataimba na kurekodi pamoja na warembo wote wa Miss Utalii Tanzania wanaoshiriki fainali za mwaka 2010.
Kibao hicho ndicho kitakachotumika katika fainali za shindano hilo zitakazofanyika Septemba mwaka huu kwa kushirikisha jumla ya warembo 60 toka kanda na mikoa mbalimbali.
Washindi wa fainali hizo za Taifa watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia na ya kimataifa 2010 na 2011 yakiwemo ya Miss Heritage World 2011,Miss Tourism University World 2011,Miss Globe International 2010,Miss United Nation 2010,Miss Tourism World 2010 na Miss University africa 2011.
Rais wa Miss Utalii alithibitisha kuwepo kwa makubaliano hayo na Diamond, ingawa msanii huyo mwenyewe hakuweza kupatikana kufafanua juu ya suala hilo.

Mwisho

No comments:

Post a Comment