STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Diamond yaja na Power 2010


Diamond Musica yaja na Power 2010

BENDI ya Diamond Musica 'Vijana Classic', imeachana na mipango ya maandalizi ya kuzindua albamu ya pili ya 'Mapenzi Kitu Gani', badala yake sasa imeelekeza nguvu katika kuandaa albamu ya tatu.
Mkurugenzi msaidizi wa bendi hiyo Perfect Kagisa, ameliambia Micharazo Mitupu kuwa kwa vile nyimbo zao albamu ya pili zilishasikika sana redioni, kwenye televisheni na katika kumbi mbalimbali, haina haja kuizindua.
"Tumeamua kuandaa albamu nyingine kwa sababu pia bendi yetu ilifanya mabadiliko kwa kuleta wanamuziki wapya, ndipo tukaona kuwa tuanze pia na vitu vipya," alisema Kagisa.
Kagisa alizitaja baadhi ya nyimbo ambazo bendi hiyo imezikamilisha kwa ajili ya albamu ya tatu kuwa ni 'Power 2010', 'Kovu', 'Supu ya Kongolo' na 'Abdulkarim'.
Alisema wanamuziki wa bendi hiyo wanajiandaa kushuti video ya wimbo wa 'Power 2010' na kwamba kazi hiyo ya kushuti itafanyika wiki ijayo ili uanze kurushwa kwenye vituo mbalimbali vya televisheni.
"Hii intro ya Diamond Musica, ndio maana tumeamua kuanza nayo na kisha nyimbo nyingine zitafuata katika mpangilio wetu wa kurekodi nyimbo za albamu ya tatu," alisema.
Diamond Musica ilitua jijini Dar es Salaam zaidi ya miaka mitatu iliyopita ikitokea Zimbabwe ikiwa na albamu ya kwanza iliyopewa jina la 'Swali' ambayo hata hivyo, haikuitambulisha vyema bendi hiyo.
Baada ya hapo wanamuziki walikuna vichwa na kuibuka na albamu ya pili ya 'Mapenzi Kitu Gani' na kuifanya uanze kukwea matawi ya juu, lakini hadi sasa albamu hiyo haijazinduliwa.
Hata hivyo, mkurugenzi huyo alisema kuwa licha ya kuandaa albamu nyingine, zile za albamu ya pili zitaendelea kupigwa kwenye kumbi za burudani na kuuzwa madukani kama kawaida.

No comments:

Post a Comment