STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 19, 2010

Wawili waiacha bendi ya Kalunde



Wanamuziki wawili wa bendi ya Kalunde ambayo iko chini ya ukurugenzi wa Deo Mwanambilimbi, wameondoka kwenda nje ya nchi kwa ajili ya kufanya shughuli za muziki
Akizungumza na Micharazo, mkurugeni huyo aliwataja wanamuziki hao kuwa ni mwimbaji Sarafina Mshindo aliyetimikia Marekani na Bonny Kamplobo (solo) ambaye amekwenda Thailand.
Mwanambilimbi alisema wanamuziki hao wameondoka baada ya kupata baraka za uongozi wa bendi na kwamba watakapomaliza mikataba yao huko waliko watarudi kuendelea kazi katika bendi hiyo.
"Sarafina anaweza kukaa Marekani kwa muda mrefu, kutokana na mkataba alioupata, lakini Kamplobo
atarudi baada ya mwezi mmoja ujao kwani atakuwa anamaliza mkataba," alisema Mwanambilimbi.
Aliongeza kuwa Kamplobo amechukuliwa na Kanku Kelly ambaye kwa sasa wanafanya naye kazi ya muziki huko Thailand na kwamba ana uhakika mkataba ukiisha atarudi Kalunde.
Alifafanua kuwa wanamuziki hao wameondoka wakati bendi hiyo ikikamilisha albamu ya kwanza ya
'Hilda' ambayo baadhi ya nyimbo zake ni 'Itumbangwewe', 'Fikiria' na 'Umenigusa Nikakugusa'.
"Hii ndio albamu ya kwanza ya bendi ya Kalunde ingawa watu wengi huwa wanadhani kwamba Uchona ni albamu ya bendi, lakini ukweli ni kwamba bendi ilianzishwa wakati albamu hii ipo tayari mitaani," alisema.
Mwanambilimbi alizitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ambazo pia zimesaidia kuiweka juu bendi hiyo kuwa ni 'Siwezi Sema', 'Mwana Mpotevu', 'Chekacheka', 'Masikitiko' na 'Anitha'.
Bendi hiyo imekuwa ikitoa burudani kila Ijumaa katika ukumbi wa New Africa Hotel na kisha humalizia shughuli za burudani Jumapili, katika ukumbi wa Giraffe Ocean View, Mbezi Beach.

No comments:

Post a Comment